JE, MTU ANAWEZAJE KUWA FREEMASONS?

Kuna wa-Freemasons wanaoshangaa kwamba hawajawahi kupata watu wanaotaka kujiunga na u-Masons.
Hii ni kwa sababu wa-Masons hufikiriwa kuwa si 'watu wema' kujiunga nao. Lakini jambo hilo haliko hivyo. Kwa miaka kadhaa sasa wa-Freemasons wamekatazwa kuwataka wengine kujiunga na udugu wao.
Tunaweza kuwasimulia marafiki zetu habari za wa-Freemasons. Tunaweza kuwaelezea ma-Freemasons wanafanya nini.
Tunaweza hata kuwaeleza tunafurahia kiasi gani kuwa wa-Freemasons lakini katu haturuhusiwi, hata kungekuwa na shinikizo kiasi gani, kuwashawishi kujiunga nasi.
Kuna sababu maalumu ya kutofanya hivyo. Na si kwamba tunataka kujiona ni watu wa kipekee. Lakini kuwa m-Masons ni jambo la dhati na makini kwelikweli.
Kujiunga na u-Freemasons ni kujikita na kuishi kwa namna fulani. Tumeorodhesha baadhi yake hapo juu - kuishi kwa heshima na uadilifu, kukubali kushirikiana na kuwajali wengine, kuaminiana, na kumwamini sana Mungu.
Hakuna mtu 'atakayeshauriwa' kuchukua uamuzi huo. Kwa hiyo kama mtu anataka kuwa m-Masons, anachotakiwa kufanya ni kuchukua fomu ya kujiunga kutoka kwa m-Masons atakayoijaza na kuirejesha kwa aliyempa fomu.
Na ataipeleka kwenye nyumba ya kukutania iliyoko eneo lake. Mkuu wa Nyumba atachagua kamati itakayomtembelea mwombaji na familia yake, ili kumfahamu na kutaka kujua kwa nini anataka kuwa mwanachama au mfuasi wa Freemasons, kumuelezea yeye na familia yake kuhusu u-Freemasons na kujibu maswali yao (familia). Kisha kamati inapitia taarifa zote za mwombaji, na nyumba inapiga kura ya kumkubali au kutomkubali kujiunga. Kama kura itakuwa ya kumkubali - na kama kawaida - nyumba itawasiliana naye na kupanga tarehe ya kile kinachoitwa 'Kuingia Kiwango cha Uanafunzi' (Entered Apprentice Degree). Mwombaji atakapomaliza digrii tatu (kwa utaratibu wao) anakuwa m-Masons na mwanachama kamili wa udugu wa u-Freemasons.
Swali: U-Freemasons ni nini nao wanaamini nini?
Jibu: U-Freemasons, Nyota ya Mashariki (Eastern Star) na vyama (taasisi) vingine vya 'siri' ni vyama visivyokuwa na maadhara katika mikutano yao.
Vyama hivi vingi huonekana vikitangaza kuwa na imani kwa Mungu.
Hata hivyo, ukiviangalia kwa undani tunaona kuwa sharti pekee si kwamba lazima mtu kuamini kuwa na imani na Mungu wa kweli na Mwenye Uzima wa Milele, lakini lazima mtu aamini kuwapo kwa 'Mwenye Mamlaka Yote' au 'Mungu muweza wa yote, ambaye ni pamoja na miungu wa Kiislamu, wa Kihindu, na dini nyingine zozote duniani. Ile hali ya kutokuwa na imani na Biblia na Ukristo na mambo mengine katika taasisi hizi, kwa namna fulani zimefungamanishwa pamoja katika imani ya Kikristo.
Ufuatao ni ulinganisho baina ya kile Biblia inachosema na msimamo rasmi wa u-Freemasons.

UOKOVU KUTOKANA NA DHAMBI:
Mtazamo wa Biblia: Yesu alikuwa kafara kwa wenye dhambi mbele ya Mungu alipoitoa damu yake na kufa kama suluhu (malipo) kwa madhambi ya wale wote wenye kuamini. (2:8-9 Waefeso 2:8-9, Warumi 5:8, Yohana 3:16).
Mtazamo wa wa-Masons: Mchakato wa kujiunga na nyumba ya kukutania unawataka Wakristo wakatae Yesu Kristo kuwa yeye ndiye pekee Bwana.
Kutokana na u-Freemasons, kuokolewa kwa mtu na hatimaye kwenda mbinguni kutakuwa ni matokeo ya kazi nzuri na alivojiendeleza yey binafsi.
Mtazamo wa Biblia: Msukumo wa kimiujiza wa Maandiko Matakatifu yaliyo na mamlaka kamili - kwamba ni kama mfano wa watu wasiotafuta ujasiri na kwamba mafundisho yao na mamlaka huwa na imani ya kweli, ya juu na yenye uamuzi wa mwisho. Biblia ni neno la Mungu (
2 Timotheo 3:16, 1Wathesalonike 2:13).
Mtazamo wa wa-Masons: Biblia ni miongoni mwa 'Vitabu vya Sheria Takatifu' ambavyo vyote vinaonekana vina umuhimu sawa kwenye u-Freemasons.
Biblia ni kitabu muhimu kadiri wale wanaodai kuwa ni Wakristo wanavyohusika, kama vile Kurani ilivyo kitabu muhimu kwa Waislamu.
Biblia haifikiriwi kuwa kitabu pekee cha Neno la Mungu, wala si kitabu pekee cha Ufunuo wa Mungu mwenyewe kwa binadamu; lakini ni kitabu kimojawapo katika vitabu vingi vinavozungumzia vyanzo vya dini. Ni mwongozo wenye uadilifu.
Biblia hutumika kwanza kama alama ya matakwa au utashi wa Mungu, ambao pia utashi huo huweza kupatikana katika vitabu vingine vitakatifu.
Waisraeli kutoka Misri 20:3). Mtume Paulo alizungumzia kuabudu masanamu kuwa ni dhambi ya kutisha) na Mtume Yohana alisema wanaoabudu masanamu watapelekwa Jehanamu (Ufunuo 21:8).
MAFUNDISHO YA MUNGU: 
Mtazamo wa Biblia: Kuna Mungu mmoja. Majina mbalimbali yanaelekeza kwa Mungu wa Israeli na kuweka bayana sifa fulani za msingi za Mungu. Kuabudu miungu mingine au kuabudu uungu mwingine ni kuabudu masanamu (
Mtazamo wa m-Masons: Wafuasi wote wa u-Freemasons lazima waamini kuwa kuna uungu. Dini mbalimbali (Ukristo, Yuda, Uislamu nk.) wanamkubali Mungu huyo huyo, isipokuwa humtaja yeye kwa majina mbalimbali. U-Freemasons huwakaribisha watu wa imani zote, hata kama wanatumia majina tofauti kwa wale 'miungu mia moja wasio na majina,’ wote wanafanya sala zao kwa Mungu mmoja ambaye ni baba wa viumbe vyote.
MAFUNDISHO YA YESU NA UTATU: 
Mtazamo wa Biblia: Yesu alikuwa Mungu lakini katika hali ya uanadamu (
Mtazamo wa m-Masons: Hakuna upekee kwa Yesu Kristo au Utatu wa Mungu ambao ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu; kwa hiyo hakuna mafundisho ya uungu wa Yesu Kristo. Hiyo inaonekana kutokuwa na ile hali ya m-Masons ya kuomba wakati wa kusali au kutaja Jina lake katika Jumba.
Majadiliano kuwa Yesu ndiyo njia pekee ya kufika kwa Mungu inakinzana na kanuni ya uvumilivu. Jina la Yesu limeachwa katika aya za Kibiblia ambazo zinatumika katika taratibu za ki-Masons. Yesu huwa yuko katika ngazi ile ile ya viongozi wengine wa dini.
Mateo 1:18-24, Yohana 1:1). Yesu ni mtu wa pili katika Utatu (Mateo 28:19, Marko 1:9-11). Akiwa duniani alikuwa binadamu (Marko 4:38, Mateo 4:2) na alikuwa na utukufu (Yohana 20:28, Yohana 1:1-2, Matendo 4:10-12). Wakristo lazima wasali kwa jina la Yesu na kumtangaza Yeye mbele ya wengine, bila kujali kuwakosea wale wasio Wakristo (Yohana 14:13-14, 1 Yohana 2:23, Matendo 4:18-20).
ASILI YA MWANADAMU NA DHAMBI: 
Mtazamo wa Biblia: Watu huzaliwa wakiwa wa asili ya dhambi, wakiwa waliopotoka na wanahitaji Mwokozi kutoka katika dhambi (Warumi 3;21, Warumi 5:21, Zaburi51:5, Waefeso2:1). Biblia inakataa kuwa kwa sababu ya Anguko, ndani yake ubinadamu kuna nafasi kwa uadilifu uliokamilika (1Yohana 1:8-10, Warumi 1:18-25).
Mazamo wa wa-Masons: Kupitia alama na nembo, wa-Masons hufundisha kuwa mtu yule hana dhambi, na ni 'jeuri tu na kwa asili ni wakosefu'.
Binadamu wanaweza kuboresha utu na tabia zao katika njia mbalimbali, ikiwa ni pamoja na matendo ya hisani, maisha ya uadilifu na matendo ya kujitolea ya kazi za kijamii.
Ubinadamu una uwezo wa kujitoa kutoka katika maisha ya kidosari na kuingia katika maisha ya ukamilifu. Maisha ya ukamilifu wa kiroho uko ndani ya wanawake na wanaume.
Wakati Mkristo anapokula kiapo cha u-Freemasons, anaapa kufuata mafundisho ambayo Mungu amekataza na kuwa ni ya dhambi:
1. Kwamba uokovu unaweza kupatikana kutokana na kazi yako nzuri.
2. Kwamba Yesu ni mmoja tu miongoni mwa mitume wanaoheshimika sana.
3. Kwamba watakaa kimya ndani ya Jengo na kutozungumza na Kristo.
4. Kwamba wanalikaribia Jengo wakiwa katika giza la kiroho na kutokujua, wakati Biblia inasema Wakristo tayari wako katika nuru, ni wana wa nuru, na wamezingirwa na Nuru ya Dunia – ambayo ni Yesu Kristo.
5. Kwa kudai Wakristo wanakula kiapo cha ki-Masons, u-Masons unaowaongoza Wakristo kwenda kukufuru na kulichukua jina la Bwana bila mafanikio.
6. U-Masons unafundisha kuwa (wasanifu wakuu wa ulimwengu), ambao wa-Masons wanaamini ni Mungu wa kweli wa ulimwengu, ni mwakilishi wa miungu katika dini zote.
7.U-Masons unawafanya Wakristo kuchukua njia ya kilimwengu katika sala zao, wakitaka jina la kutumika kwa wote litumiwe ili kwamba lisiwaudhi wasioamini ambao ni 'mabruda' wa ki-Masons.
8. Kwa kula kiapo cha ki-Masons na kushiriki katika mafundisho ya Jengo, Wakristo wanaeneza injili ya uongo kwa wanachama wa Jengo, wanaoangalia tu mpango wa u-Masons wa uokovu wa kukuwezesha kwenda mbinguni. Kwa ufuasi wao na katika aina ya taasisi, watakuwa wamehatarisha ushuhuda wao kama Wakristo.
9. Kwa kufuata wajibu wa ki-Masons, Mkristo anakubali kuruhusu uharibifu wa kiakili, kiroho na kimwili kwa wale wanaotumikia miungu na mafundisho ya uongo. Kama unavyoweza kuona, u-Masons unakataa na unakinzana na mafundisho ya kweli ya Biblia Takatifu na masuala mengine kadhaa.
U-Masons pia unawataka watu wasijishughulishe na yaliyokatazwa na Biblia. Kwa maana hiyo Mkristo hatakiwi kuwa mfuasi wa chama au taasisi yoyote ya siri ambayo ina uhusiano na Freemasons.

Imetafsiriwa na Bakari Omari Bakari 'Teacher' -0655 188666.

Post a Comment

emo-but-icon

Follow Us

Hot Reads

Recent

Comments

Side Ads

Traffic

Text Widget

Connect Us

item